Monday 29 September 2014

WELCOME TO MATEMA BEACH FESTIVAL

The Southern Highlands Sports and Culture Festival
Date: 28th , 29th and 30th November 2014
Numbers of 2014 Festival Sports 2014
1. International Ultimate Frisbee (Frisbee Tournament of Lake Nyasa )
2. Canoe (Nyasa Canoe Challenge )
3. International Mountain Bike (Race to Matema)
4. Bao ( Bao Game of Lake Nyasa)


Sport: Frisbee International Sand Tournament 2014
Location: Matema Beach Kyela in Mbeya Region TANZANIA.
Date: 29 & 30 November 2014.
Number of Playing Ground: 4
Number of Team: 6-12
Type: Team/Club & HAT
Registration Fee: 25.00 USD (Include Team T-Shirt, Two days Lunch Meals and other Entertainments
Room & Camping Accommodations: Matema Beach View Lutheran Centre.


Sport: Canoe
Location: Matema Beach Kyela in Mbeya Region TANZANIA.
Date: 29 & 30 November 2014
Competition Location: Ngonga Beach to Matema Beach Lake Nyasa shore
Number of Participants: 40
Sports Type: Single, Double and Four player Competition
Registration Fee: 25.00 USD (Include Team T-Shirt, Two days Lunch Meals and other Entertainments
Room & Camping Accommodations: Matema Beach View Lutheran Centre.


Sport: Mountain Bike
Date: 28th, 29th and 30th November 2014
Stages: 3
Total Kilomiter: 165
Days: 3
First Stage: Chimala Mbeya-Kitulo Farm Njombe
Second Stage: Kitulo Farm Njombe –Mwakaleli Busokelo Mbeya
Third Stage: Mwakaleli Busokelo Mbeya-Matema Kyela Mbeya
Registration Fee: 75.00 USD (Include T-Shirt, Three days Meals and other Entertainments
Accommodation Type for Day 1 & 2: Camping Tent.
Accommodation Type for Day 3: Camping and Room*
*Room should be booked (Should be booked in advance at Matema Beach View Lutheran Centre)


Sport: Bao Game
Location: Matema Beach Kyela in Mbeya Region TANZANIA.
Date: 29 & 30 November 2014
Competition Location: Matema Beach View Lutheran Centre
Number of Participants: 10
Accommodations: Camping Tent
Accomodation at Matema Beach
Room AccomodationCost:Tsh.20,000/= to Tsh.150,000/=
Camping Tent:Tsh.10,000/=
May Contact : Matema Beach View Lutheran Centre
Website: http://www.matemabeachview.com/
Email:matemalbcc@gmail.com,mbvlclutheran@yahoo.com
Tel: +255 684 991 030 or +255 767 552 143

Transport to MBEYA

By Air
Recommended Air Transport:
1. FastJet
2. Precision Air
3. Air Tanzania
Flight Cost Range:Tsh.40,000/= to Tsh.150,000/= (Bus connection:From Songwe International Airport to Matema Via Tukuyu ,Kyela -Ipinda:Tshs.10,000/= toTsh.15,000/=)


By Road
1. Public Buses
Cost Range:Tsh.25,000/= to Tsh.50,000/= (Bus connection from Kyela to Matema Via Ipinda Tsh.5000/=)

By Railway
1. TAZARA
Cost Range:Tsh.30,000/= to Tsh.80,000/=(Bus connection from Railway Stand to to Matema Via Tukuyu ,Kyela -Ipinda:Tshs.5,000/= toTsh.10,000/=)
Thursday 25 September 2014

MATUKIO KATIKA PICHA SAFARI YA LAKE NGOSI

 Maeneo ya uyole ya kati kibao cha coca kilichoandikwa karibu Mbeya, mahala tulipokutana washiriki wote ili tuweze kuanza safari ya pamoja kuelekea ziwa ngosi.
Vijana kutoka MBEYA YOUTH DEVELOPMENT NETWORK (VIJANA MBEYA) Steve Mwakakeke, Kelvin Paul na Christopher Mwaipopo.
Mr. Mannaseh aliekuwa Tour guide wetu ambae kwa kweli tulimuona kama mzee lakini shughuri yake ya kupanda milima vijana wengi hawakuona ndani.
Swaiba Mswahili akiwa na Rehema Joel, na pembeni ni Mr. Manaseh wakiuangalia muinuko uliokuwa mbele yao
Ni moja kati ya vibao tulivyokutana navyo tulipoingia katika msitu wa poroto, kikiwa kimeandikwa usiingie msituni, usilime msituni, usiwinde msituni, usianzishe moto na usichunge mifugo.

 Dada yetu Happy Mmila ambae ni Mtanzania lakini anasoma katika chuo cha makelele uganda, pia ni balozi mzuri sana wa mambo ya utalii alisema lazima nifike ili niweze kuwasimulia wenzangu ili waweze kufika ziwa ngosi.

 Sehemu ya kwanza ya mapumziko ya safari yetu

 Baada ya kufika juu muonekano wa ziwa ngosi ulikuwa hivi, kiukweli ni sehemu ambayo inavutia sana na kuna ubaridi saafi
 Kelvin paul, Lwitiko Mwamasika na shark wakipiga picha ya pamoja juu ya mlima.

 Wadau wakishuka kutoka juu kuelekea mahali ziwa liliko, ilituchukua muda wa kutosha ili kuweza kuyafikia maji. baada ya kushuka tukakatiza katika msitu mnene na ndipo tukafika katika kingo za ziwa Ngosi

Christopher Mwaipopo akiwa ndani ya Hifadhi ya msitu wa Poroto.

 Ukiwa juu ziwa ngosi huonekana kama ramani ya Afrika hivyo hiki ni moja kati ya vitu vyenye muonekano wa visiwa ambavyo viko viwili.
 Matukio mbali mbali yakiendelea na wadau hawakupenda kuwa mbali na matukio karibu kila mmoja alipenda japo achukue picha ama picha za mnato kama kumbukumbu

 Washiriki mbali mbali wa shindano la kukimbia na yai likiwa juu ya kijiko, kisha kijiko kinang'atwa na meno ya mbele.

 Mshindi wa shindano la kukimbia na yai akizungumza na mdhamini wa shindano hili bwana Volustano Mdee kutoka Mbeya living Lab



Sylivester Seme akipumzika baada ya safari ndefu.


 Ripoti maalum itawajia juu ya utafiti uliofanywa na wadau waliotembelea ziwa ngosi

JE NI KWELI UKIPIGA KELELE/KUITA JINA LA MTU YEYOTE UNAPOTEA?
JE NI KWELI UKINYWA MAJI YA ZIWA NGOSI UNATOKWA NA TONSES?
JE NI KWELI UKIONGEA KINYAKYUSA ZIWA LINAHAMA?

Haya yote tutakupatia majibu baada ya kufanya utafiti katika ziwa ngosi........

Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.
Wednesday 17 September 2014

CHIEF MKUU WA MBEYA AZUNGUMZIA SAFARI YA ZIWA NGOSI

 
Kutakuwa na michezo ifuatayo 1. Mchezo wa hisia (kutoa machozi) Mchezo huu utakua na washiriki nane (8) ambao watachukua namba za ushiriki kuanzia101-108. Mdhamini wa mchezo huu atakua ni FRESOWE 2. Kuziba macho nakutembea katika vibox Mchezo huu utakua na washiriki nane (8) ambao watachukua namba za ushiriki kuanzia 109-116. Mdhamini wa mchezo huu ni EGGYBUSINESSSOLUTION.BLOGSPOT.COM  3. Kutembea na yai juu ya kijiko Mchezo huu utakua na washiriki sita (6) ambao watachukua namba za ushiriki kuanzia 117-122. Mdhamini wa mchezo huu ni MBEYA LIVING LAB.  4. Kutaja vivutio visivyo julikana (naujua Mbeya kuliko wewe)  Mchezo huu utakua na washoriki kumi (10) ambao watachukua namba za ushiriki kuanzia 123-132. Mdhamini wa mchezo huu ni MBEYA HOME OF TOURISM.

Muda mchache uliopita tukafunga safari na kuelekea nyumbani kwa Chief mkuu wa wasafwa mkoa wa Mbeya Chief Mwanshinga ili kuweza kupata maelezo ya Ziwa Ngosi kwa undani kabla ya safari, alisema Ziwa hili ni la Mungu hivyo liko salama japo watu wake hulipamba kwa namna wanavyujua wao, Japo alitusihi sana tusiende na kuogelea katika ziwa lile. aliongea mengi sana ya kututia moyo na kuondokana na mila potofu zinazosemwa na wengi zaidi akasema niwatakie safari njema yenye heri na mafanikio tele.

Washiriki wote waliojipanga katika mashindano mbali mbali yatakayo kuwepo watakuwa na namba maalum za ushiriki ili waweze kutambuliwa kiurahisi, tunawaomba wote mliojiandaa kushiriki mjiandae vyema maana taasisi zilizodhamini pia zimejiandaa vyema kwa zawadi.

Maandalizi bado yanaendelea jana tulipata bahati ya kuwatembelea MBEYA FILM ALL STAR ambao wao wanajiandaa kwa VUNJA MBAVU na IGIZO KIDOGO, na leo tutakuwa MBEYA LIVING LAB.


MUHIMU
· Kufika kwa muda
· Sweta au koti kwa ajili ya baridi
· Kiatu cha safari
· Suruali au pensi (wasichana)

 NYOTE MNAKARIBISHWA



Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.
Saturday 13 September 2014

LAKE NGOSI SAFARI



ZIARA YA ZIWA NGOSI ITAKAYO FANYIKA KATIKA JIJI LA MBEYA ILI KUHAMASISHA UTALII WA NDANI NA NJE YA MKOA

Kauli Mbiu: Mbeya ni chachu ya utalii

Blog pendwa iliyojikita katika kuelimisha, kuhamasisha na kutangaza utalii na utunzaji wa mazingira katika mkoa wa Mbeya ijulikanayo kwa jina la MBEYA HOME OF TOURISM kwa kushirikiana na kamati ya utalii mkoani mbeya iliyochini ya mkuu wa mkoa ikiongozwa na mwenyekiti Mr. Msigala na taasisi mbali mbali za mkoa wa Mbeya tumeandaa safari ya kitalii (adventure tourism) itakayokuwa siku ya jumamosi tarehe 20/09/2014 ambayo itakuwa ya kuelekea ziwa Ngosi Gharama ya safari hii ni mguu wako tu, tutapita njia nzuri iliyokaa ki adventure ambayo iko uyole, kila mshiriki atachangia  Tsh 1,500 ambayo hulipwa na kila mtembeleaji katika ofisi ya TANZANIA FOREST SERVICES malengo yetu ni kuwa na watu 40 tu, safari hii ina dhumuni la:-
  •   Kuhamasisha ukuaji wa utalii wa ndani na nje ya mkoa,
  • Kutangaza vivutio vinavyo na visivyo jurikana kupitia mitandao tofauti ya ndani na nje ya mkoa
  •  Elimu kwa wakazi wa mkoa kuhusu utalii na mbinu za kukuza utalii katika mkoa wa Mbeya
  •          Elimu ya utunzaji wa mazingira ya asili na yasiyo ya asili

    KKwa mtu yeyote ama taasisi ambayo ingependa kushiriki waweza kuwasiliana nasi kwa 

    simu no: 
    0766 422703 Modesto Winfred Mratibu wa tukio

    Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.
Monday 8 September 2014

TANGAZO 27/09/2014 VIJANA WA USHIRIKA NDANI YA MATEMA BEACH


Tumepokea taarifa kutoka kwa vijana wa ushirika mji uliopo nje kidogo ya Tukuyu watakuwa na safari ya kitalii kutoka ushirika kuelekea katika ziwa nyasa. safari itakuwa tarehe 27/09/2014 kama ungependa kushiriki pamoja nao gharama ya safari itakuwa ni Tsh 10,000, wasiliana nao kwa simu no: 0754 617675 Andengulile Kapulya, imedhaminiwa na Mwegelege Library.
Tutazidi kuwafahamisha zaidi kitakachokuwa kinaendelea

Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.
Sunday 7 September 2014

MLIMA LOLEZA WAPAMBWA

 Safari ikaaza na hapa ni sehemu maarufu kama mlima kucha, ni sehemu ambayo kupanda kwake hata uwe mbishi kiasi gani lazima utapandia mikono,

 Kulia ni Mtu wa kwanza kufika kileleni katika jopo la watu sabini na tisa (79) Mr. Michael Peter (meek mil)

Omary Mwakipesile aliekuwa wa pili kufika katika kilele cha mlima loleza katika facebook ni maarufu kama Swaiba Mswahili.

Miraji Ngwata katika shindano la SIJAWAHI ONA akieleza kitu ambacho hajawahi kuona
  
 Katibu wa mbeya youth develoment network akiwa na elly bonke wakizungumza na mshindi wa shindano la kula upande wa wasichana lililojumuisha washiriki saba (7)

Mshindi wa pili Venance Shitindi katika shindano la SIJAWAHI ONA lililokuwa limedhaminiwa na mbeya home of tourism, alisema hajawahi ona mwanafunzi wa kidato cha pili hajui bara lake. Lakini mshindi wa kwanza alisema hajawahi ona kondakta au mpiga debe wa ndege, na hapa ni mr Modesto kutoka mbeya home of tourism  akimkabidhi zawadi yake, ambapo mshindi wa kwanza alijinyakulia Tshert na mshindi wa pili alijinyakulia pesa.

Igizo lililoigizwa na vijana (7)ambalo lilimhusu  kijana aliesoma kwa shida sana na kubahatika kumaliza elimu ya chuo, kutokana na uhaba wa ajira akajiingiza katika biashara haramu ya  kuuza madawa ya kulevya, anakamatwa na polisi na mwisho wake ukawa kuozea gerezani.

Neno la mwisho kutoka kwa vijana ni TUMETHUBUTU, 

 Mshindi wa kwanza wa mbio akikabidhiwa zawadi yake kutoka kwa waandaaji wa shindano hilo. alikimbia kwa muda wa dakika 44:42, mshindi wa pili elly bonke alikimbia kwa dakika 45:31 na mshindi wa tatu alikwenda kwa dakika 45:59

 Kama ilivyokuwa shida kupanda hali kadharika kushuka pia ikawa zaidi ya shida, kupanda ni lazima upandie mikono basi katika kushuka style inabadirika ni lazima makalio yatagusa chini.

 Baada ya kushuka baadhi ya washiriki wakapiga picha ya pamoja na wengine wakawa tayari wametangulia majumbani kwao.

Matukio kadhaa yaliweza kuipamba siku yetu tulipokuwa mlimani, kulikuwa na nyimbo zilizoibwa kwa lugha tofauti, mashindano ya kula kwa wavulana na wasichana, kulikuwa na igizo, na mashindano ya mbio.safari yetu ilikuwa ni ya watu 79 amabo wote waliweza kupanda na hatimae kushuka salama.

Awali ya yote tupende kutanguliza shukrani za dhati kwa Taasisi zote na wale wote walioshiriki katika tukio hili la kupanda mlima loleza, kiukweli tumejifunza mengi kutoka kwa kila mmoja kama mlivyoweza kubadirishana mawazo na kutengeneza familia moja ambayo tunaamini tutashirikiana sana katika kila jambo la maendeleo.

Tupende kutambua mchango mkubwa uliooneshwa na kituo cha radio BARAKA FM 107.6 MHz sauti ya matumaini na ukombozi, ambao walitambua umuhimu wa event hii katika mkoa wetu, hivyo kujumuika nasi mwanzo mpaka mwisho wa tukio hili, pia waliweza kurusha matangazo live kutoka mlima loleza na kuzungumza na baadhi ya washiriki.Tulianza kushuka saa 8:42 na kufika katika kituo cha 15 saa 9:21 na tukaondoka hapo saa 9:29 na kufika chini saa 10:00 jioni.

kwa mawasiliano juu ya ushauri au chochote tutumie katika email: mbeyayouthevent2014@gmail.com na simu: ELLY BONKE 0764761900
 



SAFARI YA KUPANDA MLIMA LOLEZA KUTOKA MWANZO HADI KITUO CHA 15

 Kushoto ni Mkurugenzi wa FRESOWE Tanzania, Miraji Ngwata , na Modesto Winfred wakiwa Round about iliyopo katikati ya jiji la Mbeya, wakiwasubiri washiriki wengine kutoka maneneo mbali mbali ya jiji tayari kwa maandamano.

 Walioshika bango ni wawakilishi wa Mbeya youth development network (Vijana Mbeya) kushoto ni Kelvin Paul (publi realtion officer) na kulia ni Steve Mwakakeke Katibu mkuu wa vijana Mbeya, na hapa tuko RETCO tulipoanzia maandamano kisha kuelekea njia ya hospitali ya Rufaa ielekeyo mlimani.

kushoto ni Amos Asajile,Tabitha Bugali, Steve Mwakakeke na Kelvin Paul Tukimuaga bibi yetu baaada ya kutusundikiza kutoka RETCO hadi mwanzo wa mlima Rufaa kwa juu kidogo.

 Mdogo mdogo safari ikaanza, vijana wakiwa wenye nguvu na furaha tele

 Mkurugenzi wa FRESOWE akimuonesha dada nyoka aliekuwa kajiviringa juu ya mti.

 Hawakuficha furaha zao, katikati ni mkurugenzi wa T Motion bwana Robert Elia

 Vijana wa vuvuzela wakizipiga kwa shangwe wakiongozwa na Emanuel Mwansasu baada ya kufika kituo cha 15 safari ambayo ilikuwa ngumu sana,

washiriki wakionesha furaha zao kwa mapozi mbali mbali katika picha.

Mama yetu ambae hakutaka kutuacha peke yetu, alitusindikiza mpaka juu ya mlima ambae pia ni Mwenyekiti wa YWCA Oliver Kibona akiwa na mwandishi wa habari katika kituo cha BARAKA FM dada Ikupa Mwasumbi.

Tulipofika katika kituo cha 15 ambayo ni karibu nusu ya safari, tukapata chochote kitu kilichokuwa kimeandaliwa na waandaaji wa safari hii.

Kwakuwa moja ya madhumuni yetu ilikuwa kutunza mazingira, baada ya kula tukakusanya makaratasi yote na kuyaweka sehemu moja,kisha safari ikaendelea.

Mara baada ya kupata maneno machache kutoka kwa mama Bugali, tukaanza safari yetu saa 2:23 na kufika katika kituo cha 15 saa 3:23 asubuhi.

Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.
Wednesday 3 September 2014

MAANDALIZI YANAZIDI KUPAMBA MOTO

 Tshert itakayovaliwa siku ya jumamosi ya tarehe 06/09/2014 upande wa nyuma itasomeka NITASIMAMA, NITATEMBEA KIZAZI KIPYA CHA VIJANA UTHEBUTU UNAANZIA NYUMBANI.

 Upande wa mbele wa tshert itasomeka MBEYA YOUTH EVENT 2014, 

 Vuvuzela ndogo zitakazo pigwa baada ya kufika juu kileleni ikiwa kama ishara ya furaha baada ya vijana wa jiji kuwa pamoja katika Mlima Loleza

 Hapa ni baadhi ya bendera zitakazoshikwa na washiriki wote watakao shiriki kupanda mlima, zipo za kutosha kiasi kwamba hakuna atakae kosa..

MTUSAMEHE KWA KUCHELEWE KUTOA TAARIFA KUHUSU T-SHIRT, kuhusiana na event ya kupanda MLIMA LOLEZA, siku tayari zimeisha kwa ambaye utahitaji uwe na t-shirt yenye ujumbe huu wa event, unaweza ukatuagizia ili tukutengenezee au ukatuletea T-SHIRT NYEUSI yakwako au ukatuma fedha ili ukatafutiwe t-shirt na upatiwe kabla ya ijumaa saa kumi jioni, gharama ukituletea t-shirt utaambatanisha ba Tsh 3000, na unaweza ukatuagiza tukutafutie ya aina gani, MTUSAMEHE KWA KUCHELEWESHA KUWAJULISHA, jumamosi hii haitakuwa ya kusahaulika , mawasiliano zaidi 0764761900 , na 0715850113. ukishindwa kuipata usiwaze kushiriki ni haki yako kwa mliotupa majina tayari MUNGU AWABARIKI 

Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.


WAJIBIKA ENVIRONMENT CLUB 1,YAFUNGULIWA MBEYA KATIKA SHULE YA MAPINDUZI

WAJIBIKA mpango huu unajulikana kama harakati za vijana katika uwajibikaji kiuchumi na kimazingira ili kuleta maendeleo endelevu, mradi huu unaosimamiwa na YWCA TANZANIA,YWCA MBEYA kwa ufadhili wa Y GLOBAL KFUK ambao umelenga katika humasisha vijana kuwa na uthubutu katika mambo mbalimbali,

WAJIBIKA CLUB 1,hili ndilo jina la club katika shule ya msingi mapinduzi iliyo katika jiji la mbeya ambapo mradi wa wajibika utakuwa ukifanya kazi hapo shuleni


                                             mwalimu wa shule akifungua mafunzo katika CLUB




                                       wanaclub ya mazingira wakijadiri mambo mbalimbali

mwandishi wa habari na mkufunzi wa mazingira FESTO SIKAGONAMO akisisitiza jambo


                        walimu na wanafunzi wote katika kujifunza kufahamu kuhusiana na MAZINGIRA,


                                                viongozi wa WAJIBIKA CLUB 1


                      
DEBORA NJULUMI(program officer) akiwa na wanachama wa club
shughuli ndiyo kwanza imeanza vijana wana moyo wa kujitolea na kufanya kazi, mazingira ni yetu sote

Chanzo: www.ywcambeya.blogspot.com

Welcome

Travel makes one modest, You see what a tiny place you occupy in the world. This page is dedicated to promote tourist attractions of MBEYA Tanzania

Ask a question

Name

Email

Question

Submit

Popular Posts