Tuesday 4 November 2014

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUSHIRIKIANA NA VIONGOZI WA DINI KWENYE VITA DHIDI YA UJANGILI

Waziri wa Maliasili na Utalii imeanza kushirikiana na viongozi wa dini nchini katika kuhakikisha kuwa ujangili wa Wanyamapori , biashara ya meno ya tembo na usafirishaji haramu wa wanyamapori hai unakoma kwa kuwaelimisha Viongozi wa dini zote nchini ili waweze kuwahuburia waumini wao kuacha kujihusisha na vitendo hivyo kwani ni chukizo mbele ya Mwenyezi Mungu.

Akizungumza kwenye mkutano wa Viongozi wa dini zote nchini uliofanyika jana jijini Dar es Salaam Mhe, Nyalandu alisema vita dhidi ya Ujangili vinahitaji ushirikiano wa pamoja hasa kwa viongozi wa kiroho kwani wao wana kundi kubwa la watu wanaloliongoza katika jamii kwa kuwahudumia kiroho na kimwili.

Mkutano huu ni moja ya maazimio yaliyofikiwa mwezi wa tano huu kwenye mkutano mwanzo uliofanyika jijini Dare s Salaam wa kujadili mikakati ya kutokomeza ujangili wa wanyamapori na biashara ya meno ya tembo uliohusisha Wizara ya Maliasili na Utalii, Wadau wa Kimataifa wa Maendeleo na Jumuiya za kimataifa ikiwepo UNDP NA ICCF.

Mhe. Nyalandu alisema Viongozi wa dini ni watu muhimu sana katika kuhakikisha Maliasili za taifa ikiwemo wanyamapori na misitu inalindwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho kwa kuwa hata vitabu vitakatifu na kurani vinasisitiza umuhimu wa kulinda na kuhifadhi viumbe vya Mwenyezi Mungu.

‘’Viongozi wa dini lazima muwahubuirie waumini wenu kuwa kujihusisha na ujangili ni dhambi hivyo lazima waaachanae na vitendo hivyo viovu’’ Mhe. Nyalandu alisema
Alisema watu wanaojihusisha na mauaji ya tembo na usafirishaji haramu wa wanyamapori hai ni waumini wa dini ya kikiristo na dini ya kiislaamu hivyo kama Viongozi wa dini wakikemea vitendo hivyo viovu makanisani na misikitini kwa kuwakanya waumini wao hivyo wataweza kuachana na vitendo vya ujangili.

Aidha, alisema kuwa kupitia mkutano huo, Serikali pamoja na viongozi wa dini watakuwa na sauti moja yenye nguvu ambayo waumini wa dini zote wataweza kuisikia na kuitekeleza katika mapambano ya kuhakikisha mauaji ya tembo na usafirishaji haramu wa wanyamapori hai unakoma kwa kuwa Viongozi wa dini ni watu wenye sauti yenye kugusa mioyo ya watu.

Aliongeza kuwa, Viongozi wa dini kupitia mkutano huo sio tu watashiriki kwenye vita dhidi ya Ujangili pia watakuwa mstari wa mbele kwenye masuala ya uhifadhi na uendelezwaji wa Maliasilli za taifa.

‘’Sauti za viongozi wa dini ni kubwa kuliko bunduki na ni kubwa kuliko magereza hivyo tunaamini Maliasili za taifa zitaendelea kulindwa na kuhifadhiwa kwa kushirikiano nao.’’ Mhe Nyalandu alisitiza
.
Naye , Shekhe wa Dar es Salaam ,Alhadi Musa Salumu alisema wamenyamaza kiasi cha kutosha huku vitendo viovu vikiendelea kutafuna Maliasili za Taifa hivyo ni lazima wasimamie uadilifu na hisani sio kwa binadamu tu hata kwa viumbe wengine wakiwemo Wanyama pamoja na ndege nao wanahitaji hisani ya kuishi katika mazingira yao kwa kutendewa wanavyostahili.

‘’Mwenyezi Mungu anasema kila kitu kitendewe wema hata mnyama anayestahili kuuawa sio lazima umpige risasi kumi na moja wakati kulikuwa na uwezekano wa kutumia risasi moja tu’’ Shekhe Salum alisema.

Alibainisha kuwa Wanyama wana haki ya kufurahia mazingira yao kama Mtume anavyowataka waislamu wawetendee uadilifu na hisani wanyama wote wanaoliwa na wasioliwa na sio uharamu wanaofanyiwa sasa baadhi ya Wanyamapori kwa kuwaua na kuwang’o pembe na meno yao.

Naye,Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC) Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa alisema Mungu kampa Binadamu uwezo wa kuvitawala viumbe vyote vinavyopatikana katika uso wa dunia na sio kuvipukutisha kama wanavyofanya sasa kwani hayo sio mapenzi ya Mwenyezi Mungu.

Amesema tani za magogo pamoja na biashara ya meno ya tembo zinazoendelea kusafirishwa kila kukicha ni ishara tosha kuwa baadhi ya watu hawana hofu ya Mungu hivyo wao kama viongozi wa kiroho wataendelea kuwaelimisha waumini wao na ikiwezekana kuwakemea kwani kuna binadamu wenye macho lakini hawaoni na kuna binadamu wenye masikio lakini hawasikii.

Alisema Serikali kwa kushirikiana na viongozi wa dini ni lazi wahakikishe Chama cha Haki za wanyama kinafufuliwa kwani kwa sasa Wanyama wanoishi majumbani na wanyamapori wamekuwa wakimbuna na ukatili usiovumilika hivyo lazima watetewe.

Aidha, Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Dkt. Reginald Mengi alisema kuwa mkutano huo ni muhimu sana kwani Watumishi wa Mungu ni watu wanaoaminika katika jamii na wanajukumu kubwa sana katika kuhakikisha viumbe vyote vilivyoumbwa na Mwenyezi Mungu vinaendelea kuwepo kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.

Amesema Viongozi wa dini ni lazima wawe thabiti katika vita dhidi ya Ujangili wa wanyamapori, Biashara ya meno ya tembo na usafirishaji haramu ya Wanayamapori hai kwani kwa sasa hali inatisha na wahusika ni wanaojishughulisha na vitendo hivyo ni Waumini wa dini zote za kikiristo na kiislamu.

‘’ Watumishi wa Mungu na sisi wafuasi wenu lazima tutambue Maliasili ni mali za Mwenyezi Mungu na ametupa mamlaka ya kuzitumia na si kuzimaliza kama tunavyofanya sasa hatuna haki hiyo sisi tumezikuta basi tusizitumie kwa fujo’’
Alisema Watumishi wa Mungu wana kazi kubwa ya kuwaonesha na kuwafundisha Waumini wao kuwa Mapenzi ya Mungu yanawataka watunze viumbe alivyoumba Mwenyezi Mungu na sio kuviharibu kwani hizo ni zawadi walizopewa na Mwenyezi Mungu’’

Amesema kama viongozi wa dini wakiweza kufikisha ujumbe kwa waumini wao vita hivi vitafanikiwa kwa sababu wanaaminika kwenye jamii na wana nguvu kubwa sana kwa jamii hivyo chochote wanachosema wanaaminika kwa jamii kwa sababu Waumini wa dini zote wanazungumza na Mungu kupitia wao.

‘’ Viongozi wa dini tuonesheni njia katika hili , tukeemeeni pale mnapoona hatuendi sawa kama mnaamini tunayofanya sio mapenzi ya Mwenyezi Mungu ’’ Dkt. Mengi alisisitiza

Naye Waziri kivuli wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa amesema kuwa ifike hatua sasa viongozi wa dini wakatae michango ya pesa ya watu wanaotaka kujenga makanisa kwa pesa walizozipata kupitia ujangili wa Wanyamapori kwani kufanya hivyo ni kuhalalisha ujangili kwenye nyumba za ibada.

Akiwa na kofia mbili ya uchungaji na pia ni mwanasiasa amewataka viongozi wa dini kutowanyamzia wanasiasa wanapokengeuka kwa kuhamasisha wananchi kuharibu maliasili za taifa kwa mtaji wa kura hivyo ni lazima wa wakemee kwa nguvu zao zote bila kujali cheo na hadhi ya wanasiasa hao pindi wanapofanya hivyo.

Pia amesema suala la kupambana na ujangili halina chama wala itikadi hivyo amewataka viongozi wa dini kulikemea kwenye nyumba za ibada kwani viongozi wa dini watu wenye nguvu na wanaoheshimika katika jamii.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu wa pili kulia), Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Dkt.Reginald Mengi ( wa kwanza kulia)  wakiwa katika sala kabla ya kuanza Mkutano aa Viongozi wa dini zote nchini kushirikiana kwa pamoja  kupambana na ujangili  wa Wanyamapori na usafirishaji haramu wa Wanyamapori hai, Wengine ni Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC) Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa  ( wa kushoto) akifuatiwa na Waziri kivuli wa Wizara ya  Maliasili na Utalii,  Mchungaji Peter Msigwa

 
 

Thursday 30 October 2014

WELCOME BEACO RESORT MBEYA

 
Front View BEACO Hotel 
 
Garden 
 
Reception
 
Recreation Area
 
Conference Hall 
 
Rooms  
 
Mini Super Market

This beautifully furnished country house hotel provides an exclusive, comfortable and tranquil setting in which to relax; enhanced by its peaceful situation in Mbeya with landscaped gardens and woodland, along the great northern road. Opened in 2009, Beaco Resort has maintained its period charm and friendly atmosphere.Our guests are free to enjoy our multi-award winning gardens, or to spend the day relaxing in our comfortable lounges. With numerous local attractions and beautiful walks around Mbeya, there is plenty to do for everyone all within a short distance.

A haven located just moments from most of the city’s attractions including art & cultural institutions, shopping, nightlife and entertainment. Beaco resort Hotel is just long the Tanzania Zambia main road.

The central location of the hotel makes it a perfect choice for international business travelers, NGO’s and diplomats. Being Mbeya's latest attraction with serene breathtaking unique homely environment and friendly atmosphere, Beaco resort is a place you will like to frequently visit and stay for a long time. On arrival you will be warmly met by a receptionist and have more brief of our services and facilities; definitely you will appreciate our reasonable tariffs.


Karibu Tanzania, Karibu Mbeya
Saturday 25 October 2014

Hizi ni nchi duniani ambazo raia wa Tanzania anaweza kusafiri bila visa

 
Botswana – No visa is required for a maximum stay of 90 days
Burundi – No visa is required for a maximum stay of 30 days
GAMBIA – No visa is required for a maximum stay of 90 days
Guinea – No visa is required
Kenya – No visa is required for a maximum stay of 3 months

Lesotho – No visa is required for a maximum stay of 90 days
Malawi – No visa is required for a maximum stay of 90 days
Mauritius – No visa is required for a maximum stay of 90 days
Msumbiji – No visa is required
Namibia – No visa is required for a maximum stay of 3 months

Rwanda – No visa is required for a maximum stay of 90 days.[
Afrika Kusini – No visa is required for a maximum stay of 90 days per calendar year
Swaziland – No visa is required for a maximum stay of 30 days
Uganda – No visa is required for a maximum stay of 3 months.
Zambia – No visa is required for a maximum stay of 90 days for tourists and 30 days for persons traveling on business

Zimbabwe – No visa is required for a maximum stay of 3 months
Antigua and Barbuda – No visa is required for a maximum stay of 1 month
Bahamas – No visa is required for a maximum stay of 3 months.
Barbados- No visa is required for a maximum stay of 6 months
Belize – No visa is required

British Virgin Islands- No visa is required for a maximum stay of 30 days
Cayman Islands -No visa is required of tourists for a maximum stay of 60 days or of business people for a maximum stay of 10 days
Dominica – No visa is required for a maximum stay of 6 months
Grenada -No visa is required for a maximum stay of 3 months

Haiti -No visa is required for a maximum stay of 3 months
Jamaica -No visa is required.
Montserrat -No visa is required for a maximum stay of 6 months
Saint Lucia -No visa is required for a maximum stay of 6 weeks
Saint Vincent and the Grenadines – No visa is required for a maximum stay of 1 month.

Turks and Caicos Islands – No visa is required for a maximum stay of 30 days.[10
Bangladesh – No visa is required for a maximum stay of 90 days
Hong Kong -No visa is required for a maximum stay of 90 days
Macau – No visa is required for a maximum stay of 90 days.
Malaysia -No visa is required for a maximum stay of 30 days

Philippines – No visa is required for a maximum stay of 30 days; otherwise, a visa is issued on arrival for a maximum stay of 59 days
Singapore -No visa is required for a maximum stay of 30 days
Cook Islands – No visa is required for recreation or holiday visitors for a maximum stay of 6 months. Extension permits available in the Cook Islands for stays over 31 days but less than 6 months

Fiji – No visa is required for a maximum stay of 4 months. Visitor permits issued on arrival.
Federated States of Micronesia – No visa is required for a maximum stay of 30 days if the visit is for touristic or visitors’ purposes
Vanuatu – No visa is required for a maximum stay of 30 days
Chanzo: Tabianchi blog
Thursday 23 October 2014

MAAJABU YA MUNGU RAMANI YA BARA LA AFRIKA ZIWA NGOSI

Ngosi ni ziwa la kreta (crater lake) lipatikanalo Mkoa wa Mbeya kwenye milima ya Uporoto, Wilaya ya Rungwe lipo katika nyuzi 9.008°Kusini na 33.553°Mashariki, ni ziwa la pili kwa ukubwa barani Afrika baada ya lile lililoko nchini Ethiopia. Hata hivyo, wataalamu wanasema kwamba Ziwa Ngosi lina sifa za kipekee linazolitofautisha na lile lililoko Ethiopia.

Moja ya tofauti hizo ni kwamba Ziwa Ngosi limezungukwa na milima na misitu minene tofauti na lile la Ethiopia ambalo liko eneo lililo wazi na hufikika kwa urahisi kabisa kwa gari kitu ambacho hakiwezekani kwa Ziwa Ngosi. Wataalamu wanasema kwamba kuwepo kwa ziwa hilo sehemu hiyo kunasaidia kuzuia milipuko ya mara kwa mara ya volkano kwa kuwa linasaidia kupunguza misukumo ya gesi inayojijenga chini na kuanza kutafuta upenyo wa kutokea chini ya ziwa. Kitu cha kushangaza ni muonekano wa ziwa hili linakaribia kuwa na muonekano kama ramani ya bara la afrika pamoja na visiwa vyake kama ilivyo kule njombe ambapo kuna mwamba wenye ramani ya bara la Afrika unaitwa Lwivala, uliopo katika pori la hifadhi ya msitu Lwivala kijiji cha Igodivaha Wilaya ya Njombe

ziwa hili pia lina ingiza tu maji na hali toi maji kwa sababu liko katikati ya milima hivyo kuonekana kama liko shimoni alafu halina ufukwe, ziwa hili linalopatikana katika Hifadhi ya msitu Uporoto (Poroto Ridge) yenye eneo la hekta 9,332 ipatikanayo karibu na vijiji vya Kisanga 4.3km Uyole (24.4km) na mji mdogo wa Tukuyu upatikanayo wilaya ya Rugwe. Zipo imani nyingi potofu juu ya ziwa hilo la maajabu watu husema ziwa hili lilichomwa moto na wakazi wa kijiji cha Mwakaleli kwasababu lilikuwa likileta mikosi mingi kijijini hapo ikiwemo vifo vya mara kwa mara kitu ambacho si sahihi kitaalam ziwa haliwezi kuhama, Zipo imani miongoni mwa watu kuwa ziwa ngosi watu wanapotea kimazingara, kuwapo kwa sauti za watu wasioonekana ndani ya misitu, wengine husema ziwa hilo limekuwa likigeuka rangi mara kwa mara na kuwa na rangi za kijani, bluu, nyeusi na nyeupe kitu ambacho kinawafanya waamini kuwa ziwa hilo sio la kawaida.

Chief mkuu wa wasafwa mkoa wa mbeya Chifu Rocket Masoko Mwanshinga alisema ni jambo la ajabu na kusikitisha sana kuona ziwa ngosi linafahamika sana kwa wageni kuliko wenyeji, hivyo anapenda kutoa wito kwa wadau wote wa utalii kulitangaza ziwa hili ili liweze kufahamika sana ndani na nje ya nchi. alisema jina hilo ni la kisafwa linalotokana na neno Gosi lenye maana ya kubwa hivyo kwa wasafwa walimaanisha ziwa kubwa na pia alisema maji ya ziwa lile ni maji safi na ya baraka tofauti na vile watu wanaamini.

Safari ilijumuisha washiriki 30 kutoka taasisi mbalimbali kama Mbeya Living Lab, FRESOWE, Mbeya Home of Tourism Blog, Mbeya Youth Development Network (Vijana Mbeya) na EGY business solution na watu binafsi ambao kwa ujumla ilikamilisha idadi hiyo ya watu 30.

Safari ilianza eneo la Uyole ya kati Kibao cha Coca Cola mnamo saa 2:00 asubuhi kuelekea ziwani ambapo washiriki karibu wote walikua wamewasili tayari kwa safari tukiwa tunaongozwa na kiongozi mteule kutoka Tanzania Forest Servises (TFS) ajulikanae kwa jina la Mr. Manaseh

Katika safari yetu ilitubidi kugawa makundi mawili ya watu 15 ili kurahisisha kutambuana ambapo kundi namba moja (1) lilikuwa chini ya modesto winfred na kundi namba mbili(2) lilikuwa chini ya amos asajile, hivyo washiriki wote tulifika kituo cha kwanza mnamo saa 4:30 Na kupumzika kwa muda wa dakika 20, ndipo tulipoanza safari kueleke kituo cha pili ambapo ilikuwa ndio sehemu ya juu ya milima inayolizunguka ziwa ngosi tulipumzika na kupata chakula cha mchana, mahali hapa palikuwa na upepo mwanana na baridi kali sana iliyopelekea watu wote kuvaa tena masweta yetu.

Hatukuishia hapo ndipo safari ikaanza tena na hapa ndipo kindumbwe ndumbwe kikaanza kwani ilikuwa sehemu ngumu sana ambayo ikapelekea idadi kubwa ya watu kushuka kwa kutumia makalio, baada ya kumaliza kile kilima ndipo moja kwa moja tukaingia katika ule msitu mnene mithili ya Amazon kutokana na kukosekana kwa alama zenye kuonyesha muelekeo kundi namba mbili (2)  tukapotea na kujikuta tukielekea usawa wa afrika kusini badara ya kwenda ule upande viliko visiwa. Na kibaya zaidi ni kwamba Muwapo ndani ya msitu huo hakuna simu inayoshika kutokana na kukosekana kwa mtandao hivyo ikawa ngumu kuwasiliana na kundi namba (1)  lakini tulipofika mbele tukakuta njia haionyeshi kuwa kuna watu wamepita hivyo tukarudi nyuma na kuikuta njia ambayo wenzetu walipita hivyo kundi namba moja waliwahi kufika lakini kundi namba mbili tukachelewa kidogo kufika.

Kutokana na maelezo tuliyokuwa tumepewa na Tanzania forest services nyanda za juu kusini ilikuwa ngumu kuwaruhusu watu kuogelea hivyo hakuna mdau yeyote aliyeogelea ziwani hapo kwa sababu za kiusalama. Tukapumzika kidogo na kisha tukaanza ratiba ya michezo na matukio mbali mbali kama yalivyokuwa yameandaliwa kama vile kutaja vivutio vipatikanavyo maeneo ya mkoa wa Mbeya (Naijua Mbeya Kuliko wewe), kukimbia na yai katika kijiko na shindano la hisia (kulia) ambapo washindi waliopatikana walikabidhiwa zawadi zao kutoka kwa taasisi wadhamini wa mashindano hayo, mara baada ya kumaliza hayo ndipo saa 9 jioni tukaanza safari ya kurudi kwa makundi kama awali.

Tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu aliyekuwa pamoja nasi katika safari yetu kwani wote tulikwenda salama na kurudi salama hakuna hata aliyeumia katika safari hii. Pia tupende kutoa shukrani zetu za dhati kwa taasisi wasiriki, kamati ya utalii ya mkoa wa mbeya na wadau wote walioshiriki ambao kiukweli kutokana na wingi wao itakuwa ngumu kuwataja kwa majina.

Kuna baadhi ya vitu ambavyo vinakwamisha sana kukua ama kufahamika kwa ziwa ngosi miongoni mwa vitu hivyo ni pamoja na, Miundo mbinu mibovu ambayo hupelekea watalii kushindwa kufika kwa urahisi katika eneo husika, Viongozi wachache wa safari (tour guides), Matangazo ya kivutio, Taarifa na maelezo hafifu ya kivutio, Makosa ya matamshi ya jina. Pamoja na hayo Jitihada muhimu zinahitajika ikiwemo kuzuia mmomonyoko wa udongo unaosababisha udongo kuingia ziwani hivyo kupunguza kina cha ziwa, kujenga angalau ngazi zenye sehemu za kujishikiria katika baadhi ya maeneo ambayo ni tatanishi/magumu kupanda ama kushuka, vyombo mbali mbali vya habari kujitokeza kwa wingi kulitangaza ziwa ngosi, pia kujenga kijisehemu kidogo ambacho kitatoa huduma muhimu ikiwemo chakula na vinywaji.

 Muonekano wa ziwa ngosi muwapo sehemu ya  juu ya milima iliyolizunguka ziwa hilo

Jiwe linalopatikana njombe lenye muonekano wa ramani ya bara la afrika

Karibu Tanzania, Karibu Mbeya
Tuesday 21 October 2014

PRIVATE SECTOR INVESTMENTS NEEDED TO BOOST TOURISM IN TANZANIA

SUBSTANTIAL investments are needed to enhance the contribution of the tourism sector to the economy and for improved living standards of the people.
Tourism industry is the vehicle for economic development and employment creation. The sector is currently the top foreign exchange earner after overtaking gold exports which suffered global price decline and reduced output. 

According to Bank of Tanzania (BoT) latest monthly economic review, earnings from tourism reached 1.972 billion US dollars in the year between July 2013 and June 2014 up from 1.757 billion US dollars from the previous period. Gold exports earnings from the same period were calculated at about 1.6 billion US dollars.
Speaking to students shortly before commencing a tour to Selous Game Reserve last week, the Minister of Tourism and Natural Resources, Mr Lazaro Nyalandu said there were abundant opportunities in the tourism sector that called for more investments particularly from the private sector.

The base for future development of tourism as a vehicle for economic development, employment creation is now on the hands of the private sector, he said.
"Tourists are prepared to spend more money in one destination than they would if they visited another, as long as they feel they are getting value for money. It is not true that a destination that is expensive will not thrive," he said.
Mr Nyalandu cited the southern part of the country as the destination that offers plenty of opportunities for investors, particularly domestic, like building hotels and campsites and other cultural goods which could earn substantial incomes.

Tourist experience is not measured alone on the beach or wildlife product, rather it is the whole continuum that starts when the tourist first arrives in the country until the moment they leave.
And it extends beyond this all the way back to their place of origin including flight connections and schedules are an important part of the travel experience too.

"I invite investors to take advantage of the abundant opportunities in the southern part of the country, where the TAZARA Railway cut across to invest in hotels and lodges as well as other 2001, sorts of infrastructures to host the increasing number of tourists in the country," he said.
Statistics from the Tanzania Tourism Board (TTB) shows that in 2012, a target of one million tourists was reached with expectations of hitting 1.5 million mark in 2015. All these call for increased investments in the tourism infrastructures to cater for the increased demand.
In 2013 tourists who came to the country for recreational reasons were 890,000 and of those 65,922 came for business tourism and the number has been increasing every year.

"Where the service industry is strong, it signifies a vibrant economic growth of the country," he said, calling for the improved services in the hotel sector in order to meet the international standards.
Commenting on the TAZARA railway that crosses the southern part of the country, Mr Nyalandu said the railway offers huge potential in promoting tourism industry in the country.
Thousands of tourists are among the millions of passengers ferried by the 1860 kilometres TAZARA rail line from Dar es Salaam to New Kapirimposhi in Zambia. It crosses in some of the most unique and spectacular tourist sites. Last year, the country registered a 1.73 per cent increase of tourist arrivals to 1,095,884 from 1,077,058 in 2012.

During the period, foreign exchange earnings from industry climbed to 1.88 billion US dollars up from 1.7 billion US dollars in the preceding year.
The Selous Game Reserve Manager, Mr Benson Kibonde, urged students who toured the game reserve to cultivate the 'love for tourist attractions' as a way forward to become real investors and promoters of tourism investments.

The Chinese Ambassador to Tanzania, Dr Lu Youqing said at the event that apart from promoting economic growth, TAZARA was an important symbol for improving conservation in the country's largest wildlife reserves where it crosses.
The railway line starts from Dar es Salaam through Kazimzumbwi forest, one of the oldest forest in the world and the savannah wooded plain, where the major southern national parks of Mikumi, Udzungwa and Selous Game Reserve are located.
From there, TAZARA crosses the Great Ruaha River, towards Kilombero Flood Plains. Then it passes through tunnels under Udzungwa Mountain ranges and adjoining Kipengere Ranges to Makambako Plateau.

From Makambako the train runs on the foot of Kipengere Ranges and at the edge of Rift Valley to Mbeya. From Mbeya the train passes though smaller train stations of Mbalizi, Songwe, the Uporoto Ranges of Shikula, Mlowo, Vwawa before it arrives at Tunduma.
TAZARA Acting Managing Director Ronald Phiri said the railway not only eases mobility for some of the most disadvantaged rural communities in Tanzania and Zambia, but also provides a public railway service that is very predictable, reliable, safe and convenient.
Therefore, greater public-private sector cooperation and coordination is required in order to plan, promote, market and regulate the tourism industry in a manner that will ultimately prove to be sustainable and successful.

Tanzania is widely recognised to have unparalleled tourism potential both in terms of abundance and variety of its attractions.
The country is best known as the "Land of Kilimanjaro, Zanzibar and The Serengeti, to describe it as the home to Africa's highest mountain and the tallest freestanding mountain in the world; Ngorongoro Crater - the largest unbroken caldera in the world which is renowned for its abundance and variety of species of wildlife and The Serengeti, where the largest animal migration in the world takes place.

Source Ukarimu Tz blog
Sunday 12 October 2014

WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA (TFS) WAHIMIZA WANANCHI KOTE NCHINI KUSHIRIKI KATIKA UFUGAJI WA NYUKI ILI KUONGEZA VIPATO VYAO NA KUCHANGIA KATIKA KUKUZA UCHUMI WA TAIFA.

Hayo yamesemwa na Afisa Ufugaji Nyuki Mwandamizi wa wakala huo Bw. Steven Msemo leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliolenga kuhamasisha jamii kushiriki katika ufaugaji wa nyuki.

Akifafanua Msemo amebainisha kuwa mizinga ya nyuki takribani 14,000 imetengenezwa na kugawiwa wananchi wanaoishi jirani na Misitu ikiwa ni moja ya mikakati ya Serikali katika kukuza sekta hiyo.

“Wakala wa Huduma za misitu Tanzania kama Taasisi inayo mizinga 3,870 iliyo katika manzuki mbalimbali katika kanda saba na katika mashamba ya miti kwa lengo la kuzalisha na sehemu ya mafunzo kwa jamii “alisisitiza Msemo

Katika kuwajengea uwezo wananchi Msemo amebainisha kuwa Wataalamu wa ufugaji nyuki wamekuwa wakiwajengea uwezo wananchi kwa kuwapa mbinu za kusimamia makundi ya nyuki na kuzalisha malkia ili kuondokana na mazoea ya kutundika mizinga na kuacha hadi kipindi cha mavuno.

Aidha, Wakala umekuwa ukihamasisha asasi zinazojikita na kutengeneza vifaa vya ufugaji nyuki kuzingatia utaalamu na vipimo vya mizinga.

Tanzania ni moja kati ya nchi zenye utajiri mkubwa wa makundi ya nyuki yenye uwezo wa kuzalisha asali na mazao mengine ya nyuki mfano Nta,Gundi ya nyuki na chavua.

Chanzo: Mali Asili Zetu

CHANZO CHA MAJI NGAZI SITINI (60)


 Hapa  ndipo tunapoingilia na ndipo mahali zilipoanzia Ngazi sitini (60) zinazoelekea katika chanzo cha Maji NGAZI SITINI (60), kushoto na kulia ni miti ambayo imeshonana na kuweka ukuta wa maua uliofanya mahali hapa kuwa na mvuto wa aina yake.

Wadau wa utalii nlioongozana nao kuelekea katika chanzo cha maji NGAZI SITINI (60) Bwana Kelvin Paul (kushoto) na Lwitiko Mwamasika (kulia)wakiwa wamesimama katika lango la kuingilia katika chanzo hicho ambalo linafungwa muda wote ili kulinda usalama wa maji haya.

 Bwana Kelvin Paul na Lwitiko Mwamasika wakiwa katika zoezi la kuzihesabu Ngazi ili kuthibitisha kama ni kweli ziko sitini (60), mara baada ya kuzihesabu tukakuta zinatimia idadi hiyo hiyo ya sitini (60).
 Na huu ni moja ya muonekano ya msitu upatikanao katika chanzo hiki, kiukweli ni wenye kupendeza na rangi yake ni kijani kibichi.

 Na huu ni upande wa pili wa msitu huu, ambao umeshonana sana.

Mara baada ya kutoka katika kile chanzo cha maji NGAZI SITINI (60) tukasonga mbele zaidi ambapo tulikuta bomba hii ambayo imetoka katika chanzo asilia na maji yake ni masafi, ya baridi, na ni matamu sana, na hapa ni Bwana lwitiko akikinga maji ya kunywa ili tuendelee na safari.

Katika vyanzo vya maji tulivyopata bahati ya kuvitembelea ikiwemo ibale na izumbwe hiki ndicho chanzo cha maji ambacho kimetunzwa na kulindwa kwa hali ya juu sana, ukiwa katika mazingira ya karibu hata kabla hujafika katika zile ngazi unakuta mazingiza yake ni safi na yenye kupendeza sana kwani unafanywa usafi kila siku na hatukukuta aina yoyote ya takataka.

Chanzo hiki cha maji kinapatikana katika njia ielekeayo Ituha kwa kuingilia Ilomba.

Tuyatunze mazingira Yetu kwa afya zetu.

Karibu Tanzania, Karibu Mbeya
Monday 29 September 2014

WELCOME TO MATEMA BEACH FESTIVAL

The Southern Highlands Sports and Culture Festival
Date: 28th , 29th and 30th November 2014
Numbers of 2014 Festival Sports 2014
1. International Ultimate Frisbee (Frisbee Tournament of Lake Nyasa )
2. Canoe (Nyasa Canoe Challenge )
3. International Mountain Bike (Race to Matema)
4. Bao ( Bao Game of Lake Nyasa)


Sport: Frisbee International Sand Tournament 2014
Location: Matema Beach Kyela in Mbeya Region TANZANIA.
Date: 29 & 30 November 2014.
Number of Playing Ground: 4
Number of Team: 6-12
Type: Team/Club & HAT
Registration Fee: 25.00 USD (Include Team T-Shirt, Two days Lunch Meals and other Entertainments
Room & Camping Accommodations: Matema Beach View Lutheran Centre.


Sport: Canoe
Location: Matema Beach Kyela in Mbeya Region TANZANIA.
Date: 29 & 30 November 2014
Competition Location: Ngonga Beach to Matema Beach Lake Nyasa shore
Number of Participants: 40
Sports Type: Single, Double and Four player Competition
Registration Fee: 25.00 USD (Include Team T-Shirt, Two days Lunch Meals and other Entertainments
Room & Camping Accommodations: Matema Beach View Lutheran Centre.


Sport: Mountain Bike
Date: 28th, 29th and 30th November 2014
Stages: 3
Total Kilomiter: 165
Days: 3
First Stage: Chimala Mbeya-Kitulo Farm Njombe
Second Stage: Kitulo Farm Njombe –Mwakaleli Busokelo Mbeya
Third Stage: Mwakaleli Busokelo Mbeya-Matema Kyela Mbeya
Registration Fee: 75.00 USD (Include T-Shirt, Three days Meals and other Entertainments
Accommodation Type for Day 1 & 2: Camping Tent.
Accommodation Type for Day 3: Camping and Room*
*Room should be booked (Should be booked in advance at Matema Beach View Lutheran Centre)


Sport: Bao Game
Location: Matema Beach Kyela in Mbeya Region TANZANIA.
Date: 29 & 30 November 2014
Competition Location: Matema Beach View Lutheran Centre
Number of Participants: 10
Accommodations: Camping Tent
Accomodation at Matema Beach
Room AccomodationCost:Tsh.20,000/= to Tsh.150,000/=
Camping Tent:Tsh.10,000/=
May Contact : Matema Beach View Lutheran Centre
Website: http://www.matemabeachview.com/
Email:matemalbcc@gmail.com,mbvlclutheran@yahoo.com
Tel: +255 684 991 030 or +255 767 552 143

Transport to MBEYA

By Air
Recommended Air Transport:
1. FastJet
2. Precision Air
3. Air Tanzania
Flight Cost Range:Tsh.40,000/= to Tsh.150,000/= (Bus connection:From Songwe International Airport to Matema Via Tukuyu ,Kyela -Ipinda:Tshs.10,000/= toTsh.15,000/=)


By Road
1. Public Buses
Cost Range:Tsh.25,000/= to Tsh.50,000/= (Bus connection from Kyela to Matema Via Ipinda Tsh.5000/=)

By Railway
1. TAZARA
Cost Range:Tsh.30,000/= to Tsh.80,000/=(Bus connection from Railway Stand to to Matema Via Tukuyu ,Kyela -Ipinda:Tshs.5,000/= toTsh.10,000/=)
Thursday 25 September 2014

MATUKIO KATIKA PICHA SAFARI YA LAKE NGOSI

 Maeneo ya uyole ya kati kibao cha coca kilichoandikwa karibu Mbeya, mahala tulipokutana washiriki wote ili tuweze kuanza safari ya pamoja kuelekea ziwa ngosi.
Vijana kutoka MBEYA YOUTH DEVELOPMENT NETWORK (VIJANA MBEYA) Steve Mwakakeke, Kelvin Paul na Christopher Mwaipopo.
Mr. Mannaseh aliekuwa Tour guide wetu ambae kwa kweli tulimuona kama mzee lakini shughuri yake ya kupanda milima vijana wengi hawakuona ndani.
Swaiba Mswahili akiwa na Rehema Joel, na pembeni ni Mr. Manaseh wakiuangalia muinuko uliokuwa mbele yao
Ni moja kati ya vibao tulivyokutana navyo tulipoingia katika msitu wa poroto, kikiwa kimeandikwa usiingie msituni, usilime msituni, usiwinde msituni, usianzishe moto na usichunge mifugo.

 Dada yetu Happy Mmila ambae ni Mtanzania lakini anasoma katika chuo cha makelele uganda, pia ni balozi mzuri sana wa mambo ya utalii alisema lazima nifike ili niweze kuwasimulia wenzangu ili waweze kufika ziwa ngosi.

 Sehemu ya kwanza ya mapumziko ya safari yetu

 Baada ya kufika juu muonekano wa ziwa ngosi ulikuwa hivi, kiukweli ni sehemu ambayo inavutia sana na kuna ubaridi saafi
 Kelvin paul, Lwitiko Mwamasika na shark wakipiga picha ya pamoja juu ya mlima.

 Wadau wakishuka kutoka juu kuelekea mahali ziwa liliko, ilituchukua muda wa kutosha ili kuweza kuyafikia maji. baada ya kushuka tukakatiza katika msitu mnene na ndipo tukafika katika kingo za ziwa Ngosi

Christopher Mwaipopo akiwa ndani ya Hifadhi ya msitu wa Poroto.

 Ukiwa juu ziwa ngosi huonekana kama ramani ya Afrika hivyo hiki ni moja kati ya vitu vyenye muonekano wa visiwa ambavyo viko viwili.
 Matukio mbali mbali yakiendelea na wadau hawakupenda kuwa mbali na matukio karibu kila mmoja alipenda japo achukue picha ama picha za mnato kama kumbukumbu

 Washiriki mbali mbali wa shindano la kukimbia na yai likiwa juu ya kijiko, kisha kijiko kinang'atwa na meno ya mbele.

 Mshindi wa shindano la kukimbia na yai akizungumza na mdhamini wa shindano hili bwana Volustano Mdee kutoka Mbeya living Lab



Sylivester Seme akipumzika baada ya safari ndefu.


 Ripoti maalum itawajia juu ya utafiti uliofanywa na wadau waliotembelea ziwa ngosi

JE NI KWELI UKIPIGA KELELE/KUITA JINA LA MTU YEYOTE UNAPOTEA?
JE NI KWELI UKINYWA MAJI YA ZIWA NGOSI UNATOKWA NA TONSES?
JE NI KWELI UKIONGEA KINYAKYUSA ZIWA LINAHAMA?

Haya yote tutakupatia majibu baada ya kufanya utafiti katika ziwa ngosi........

Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.
Wednesday 17 September 2014

CHIEF MKUU WA MBEYA AZUNGUMZIA SAFARI YA ZIWA NGOSI

 
Kutakuwa na michezo ifuatayo 1. Mchezo wa hisia (kutoa machozi) Mchezo huu utakua na washiriki nane (8) ambao watachukua namba za ushiriki kuanzia101-108. Mdhamini wa mchezo huu atakua ni FRESOWE 2. Kuziba macho nakutembea katika vibox Mchezo huu utakua na washiriki nane (8) ambao watachukua namba za ushiriki kuanzia 109-116. Mdhamini wa mchezo huu ni EGGYBUSINESSSOLUTION.BLOGSPOT.COM  3. Kutembea na yai juu ya kijiko Mchezo huu utakua na washiriki sita (6) ambao watachukua namba za ushiriki kuanzia 117-122. Mdhamini wa mchezo huu ni MBEYA LIVING LAB.  4. Kutaja vivutio visivyo julikana (naujua Mbeya kuliko wewe)  Mchezo huu utakua na washoriki kumi (10) ambao watachukua namba za ushiriki kuanzia 123-132. Mdhamini wa mchezo huu ni MBEYA HOME OF TOURISM.

Muda mchache uliopita tukafunga safari na kuelekea nyumbani kwa Chief mkuu wa wasafwa mkoa wa Mbeya Chief Mwanshinga ili kuweza kupata maelezo ya Ziwa Ngosi kwa undani kabla ya safari, alisema Ziwa hili ni la Mungu hivyo liko salama japo watu wake hulipamba kwa namna wanavyujua wao, Japo alitusihi sana tusiende na kuogelea katika ziwa lile. aliongea mengi sana ya kututia moyo na kuondokana na mila potofu zinazosemwa na wengi zaidi akasema niwatakie safari njema yenye heri na mafanikio tele.

Washiriki wote waliojipanga katika mashindano mbali mbali yatakayo kuwepo watakuwa na namba maalum za ushiriki ili waweze kutambuliwa kiurahisi, tunawaomba wote mliojiandaa kushiriki mjiandae vyema maana taasisi zilizodhamini pia zimejiandaa vyema kwa zawadi.

Maandalizi bado yanaendelea jana tulipata bahati ya kuwatembelea MBEYA FILM ALL STAR ambao wao wanajiandaa kwa VUNJA MBAVU na IGIZO KIDOGO, na leo tutakuwa MBEYA LIVING LAB.


MUHIMU
· Kufika kwa muda
· Sweta au koti kwa ajili ya baridi
· Kiatu cha safari
· Suruali au pensi (wasichana)

 NYOTE MNAKARIBISHWA



Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.
Saturday 13 September 2014

LAKE NGOSI SAFARI



ZIARA YA ZIWA NGOSI ITAKAYO FANYIKA KATIKA JIJI LA MBEYA ILI KUHAMASISHA UTALII WA NDANI NA NJE YA MKOA

Kauli Mbiu: Mbeya ni chachu ya utalii

Blog pendwa iliyojikita katika kuelimisha, kuhamasisha na kutangaza utalii na utunzaji wa mazingira katika mkoa wa Mbeya ijulikanayo kwa jina la MBEYA HOME OF TOURISM kwa kushirikiana na kamati ya utalii mkoani mbeya iliyochini ya mkuu wa mkoa ikiongozwa na mwenyekiti Mr. Msigala na taasisi mbali mbali za mkoa wa Mbeya tumeandaa safari ya kitalii (adventure tourism) itakayokuwa siku ya jumamosi tarehe 20/09/2014 ambayo itakuwa ya kuelekea ziwa Ngosi Gharama ya safari hii ni mguu wako tu, tutapita njia nzuri iliyokaa ki adventure ambayo iko uyole, kila mshiriki atachangia  Tsh 1,500 ambayo hulipwa na kila mtembeleaji katika ofisi ya TANZANIA FOREST SERVICES malengo yetu ni kuwa na watu 40 tu, safari hii ina dhumuni la:-
  •   Kuhamasisha ukuaji wa utalii wa ndani na nje ya mkoa,
  • Kutangaza vivutio vinavyo na visivyo jurikana kupitia mitandao tofauti ya ndani na nje ya mkoa
  •  Elimu kwa wakazi wa mkoa kuhusu utalii na mbinu za kukuza utalii katika mkoa wa Mbeya
  •          Elimu ya utunzaji wa mazingira ya asili na yasiyo ya asili

    KKwa mtu yeyote ama taasisi ambayo ingependa kushiriki waweza kuwasiliana nasi kwa 

    simu no: 
    0766 422703 Modesto Winfred Mratibu wa tukio

    Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.
Monday 8 September 2014

TANGAZO 27/09/2014 VIJANA WA USHIRIKA NDANI YA MATEMA BEACH


Tumepokea taarifa kutoka kwa vijana wa ushirika mji uliopo nje kidogo ya Tukuyu watakuwa na safari ya kitalii kutoka ushirika kuelekea katika ziwa nyasa. safari itakuwa tarehe 27/09/2014 kama ungependa kushiriki pamoja nao gharama ya safari itakuwa ni Tsh 10,000, wasiliana nao kwa simu no: 0754 617675 Andengulile Kapulya, imedhaminiwa na Mwegelege Library.
Tutazidi kuwafahamisha zaidi kitakachokuwa kinaendelea

Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.
Sunday 7 September 2014

MLIMA LOLEZA WAPAMBWA

 Safari ikaaza na hapa ni sehemu maarufu kama mlima kucha, ni sehemu ambayo kupanda kwake hata uwe mbishi kiasi gani lazima utapandia mikono,

 Kulia ni Mtu wa kwanza kufika kileleni katika jopo la watu sabini na tisa (79) Mr. Michael Peter (meek mil)

Omary Mwakipesile aliekuwa wa pili kufika katika kilele cha mlima loleza katika facebook ni maarufu kama Swaiba Mswahili.

Miraji Ngwata katika shindano la SIJAWAHI ONA akieleza kitu ambacho hajawahi kuona
  
 Katibu wa mbeya youth develoment network akiwa na elly bonke wakizungumza na mshindi wa shindano la kula upande wa wasichana lililojumuisha washiriki saba (7)

Mshindi wa pili Venance Shitindi katika shindano la SIJAWAHI ONA lililokuwa limedhaminiwa na mbeya home of tourism, alisema hajawahi ona mwanafunzi wa kidato cha pili hajui bara lake. Lakini mshindi wa kwanza alisema hajawahi ona kondakta au mpiga debe wa ndege, na hapa ni mr Modesto kutoka mbeya home of tourism  akimkabidhi zawadi yake, ambapo mshindi wa kwanza alijinyakulia Tshert na mshindi wa pili alijinyakulia pesa.

Igizo lililoigizwa na vijana (7)ambalo lilimhusu  kijana aliesoma kwa shida sana na kubahatika kumaliza elimu ya chuo, kutokana na uhaba wa ajira akajiingiza katika biashara haramu ya  kuuza madawa ya kulevya, anakamatwa na polisi na mwisho wake ukawa kuozea gerezani.

Neno la mwisho kutoka kwa vijana ni TUMETHUBUTU, 

 Mshindi wa kwanza wa mbio akikabidhiwa zawadi yake kutoka kwa waandaaji wa shindano hilo. alikimbia kwa muda wa dakika 44:42, mshindi wa pili elly bonke alikimbia kwa dakika 45:31 na mshindi wa tatu alikwenda kwa dakika 45:59

 Kama ilivyokuwa shida kupanda hali kadharika kushuka pia ikawa zaidi ya shida, kupanda ni lazima upandie mikono basi katika kushuka style inabadirika ni lazima makalio yatagusa chini.

 Baada ya kushuka baadhi ya washiriki wakapiga picha ya pamoja na wengine wakawa tayari wametangulia majumbani kwao.

Matukio kadhaa yaliweza kuipamba siku yetu tulipokuwa mlimani, kulikuwa na nyimbo zilizoibwa kwa lugha tofauti, mashindano ya kula kwa wavulana na wasichana, kulikuwa na igizo, na mashindano ya mbio.safari yetu ilikuwa ni ya watu 79 amabo wote waliweza kupanda na hatimae kushuka salama.

Awali ya yote tupende kutanguliza shukrani za dhati kwa Taasisi zote na wale wote walioshiriki katika tukio hili la kupanda mlima loleza, kiukweli tumejifunza mengi kutoka kwa kila mmoja kama mlivyoweza kubadirishana mawazo na kutengeneza familia moja ambayo tunaamini tutashirikiana sana katika kila jambo la maendeleo.

Tupende kutambua mchango mkubwa uliooneshwa na kituo cha radio BARAKA FM 107.6 MHz sauti ya matumaini na ukombozi, ambao walitambua umuhimu wa event hii katika mkoa wetu, hivyo kujumuika nasi mwanzo mpaka mwisho wa tukio hili, pia waliweza kurusha matangazo live kutoka mlima loleza na kuzungumza na baadhi ya washiriki.Tulianza kushuka saa 8:42 na kufika katika kituo cha 15 saa 9:21 na tukaondoka hapo saa 9:29 na kufika chini saa 10:00 jioni.

kwa mawasiliano juu ya ushauri au chochote tutumie katika email: mbeyayouthevent2014@gmail.com na simu: ELLY BONKE 0764761900
 



Welcome

Travel makes one modest, You see what a tiny place you occupy in the world. This page is dedicated to promote tourist attractions of MBEYA Tanzania

Ask a question

Name

Email

Question

Submit

Popular Posts