Saturday 28 June 2014

KARIBU UPUMZIKE KATIKA FUKWE ZA ZIWA LA TATU KWA UKUBWA AFRIKA.


 Nyumba ya kupumzikia uwapo katika fukwe za ziwa nyasa nyumba hizi huitwa msonge.

Muonekano wa wimbi katika ziwa Nyasa.

 Maji ya ziwa nyasa ni masafi kiasi kwamba unaweza kuona mchanga wake.

Pembezoni kuna safu za milima livingstone iliyosheheni misitu yenye rasilimanyi nyingi sana.

Ziwa Nyasa ni moja kati ya maziwa yenye hadhi kubwa sana duniani, Afrika na Tanzania kwa ujumla, Ziwa hili katika makala mbalimbali za dunia limekuwa likishika nafasi kwanzia ya saba (7) hadi ya kumi (10) kulingana na makala husika kwa mfano the times atlas of the world katika orodha yao wanasema ziwa hili ni la tisa (9) kwa ukubwa duniani, kutoka wikipedia ni ziwa la Tano kwa kuwa na kina kirefu sana duniani. katika tovuti ya 10most today ziwa nyasa limewekwa ni ziwa la tisa (9), katika tovuti ya fact monster ni ziwa la kumi (10)  na pia katika maps of the world ni ziwa la (8) kwa ukubwa duniani.

Katika afrika ziwa nyasa ni ziwa la tatu kwa ukubwa, baada ya ziwa Victoria, na Tanganyika chanzo ni wikipedia.

Pia ziwa Nyasa ni moja kati ya maziwa yenye sifa ya kuwa na aina nyingi za samaki ni (zaidi ya 1500).


Karibu Tanzania, Karibu Mbeya.

0 comments:

Post a Comment

Welcome

Travel makes one modest, You see what a tiny place you occupy in the world. This page is dedicated to promote tourist attractions of MBEYA Tanzania

Ask a question

Name

Email

Question

Submit

Popular Posts