Wednesday 25 June 2014

HALI YA HEWA YA MANOW KWA SIKU MBILI ZILIZOPITA.

Baadhi ya maeneo yakiwa yamefunikwa na ukungu mzito.  

 Maeneo ya barabarani pia hali ikawa ni ile ile.

 Majengo ya shule pamoja na majengo ya walimu yakiwa hayaonekani vizuri

ulikuwa huwezi kuiona lwangwa kama ilivyozoeleka siku zote.

Mwezi wa sita ni mwezi wenye baridi sana katika maeneo mbali mbali ya mkoa wa mbeya, ukiwa katika wilaya ya Rungwe hutakaa ukaacha kuvaa sweta kwa sababu ya baridi yake. 

Haya ni maeneo ya shule ya seminari  manow ambayo kwa muda wa siku mbili wakazi wake hawakubahatika kuliona jua kwa sababu ukungu ulitanda anga.

kwa wale mpendao kubadirisha hali ya hewa mkiyachoka maeneo ya joto, karibuni sana  mbeya japo kwa siku moja upunguze matumizi ya viyoyozi.



0 comments:

Post a Comment

Welcome

Travel makes one modest, You see what a tiny place you occupy in the world. This page is dedicated to promote tourist attractions of MBEYA Tanzania

Ask a question

Name

Email

Question

Submit

Popular Posts