Sunday, 31 August 2014
SHEREHE YA MATAMBIKO KABILA LA WASAFWA, MSITU WA IGANJO
Kwa mbali ni Msitu wa Iganjo ambao hutumika kama sehemu ya matambiko iliyoko huko igawilo.
kulia ni Muwakilishi John Chilambo, na katikati ni Chifu Rocket Mwanshinga na wasaidizi wake.
Mh. Joseph Mbilinyi (mbunge wa Jiji la Mbeya) na Chifu wakipiga picha ya pamoja
Picha ya pamoja ya chifu, wasaidizi wake na wageni waalikwa
Njuga zinazotumika kuchezea ngoma; huvaliwa miguuni ambazo husaidia sana kuleta radha ya ngoma.
Wakina mama wakicheza ngoma ijulikanayo kwa jina la Mbeta
Wanaume wakicheza Mbeta,
Ishara ya kidoogo inayotumiwa na hao mapacha, ikimaanisha "kukumbukwa angalau kidogo" hasa ikiwalenga viongozi
mapacha wakiwa na Mh. Joseph Mbilinyi, na muwakilishi wa mbeya home of tourism modesto
- kuwakumbuka ndugu waliokufa
- matambiko kama kuomba mvua, amani uchaguzi, magojwa biashara na mengine
- sherehe inayohusisha wasafwa wote na wageni waalikwa kufurahi kwa pamoja.
- hotuba ya chifu
Sherehe hio huongozwa na chifu (mwene) wa kisafwa anaetambulika kwa jina la Mwene Rocketi Mwanshinga ambaye ndio chifu mkuu wa wasafwa wote. chifu huyu alisema tangu apate uchifu huo hajawahi kunyoa nywele
Pia sherehe hiyo hufanyika katika msitu uitwao Iganjo upatikanao maeneo ya Uyole Igawilo. Msitu huo unalindwa kijadi na unamaajabu mengi sana kuna sehemu ambazo huruhusiwi kupiga picha kwa sababu ya taratibu za msitu huo.
Wageni mbalimbali huarikwa katika sherehe hizo bila kujali kabila wala dini.
Karibu Tanzania karibu Mbeya.
Subscribe to:
Post Comments
(Atom)
Welcome
Travel makes one modest, You see what a tiny place you occupy in the
world. This page is dedicated to promote tourist attractions of MBEYA
Tanzania





WHO IS TATUNYI.? this mistake shows that you are not serious
ReplyDelete